Mtu wa kawaida anayetumia simu hushika simu yake mara 2617 kwa siku kutokana na uchunguzi uliofanywa na Dscout research.
Mara nyingi ikiwa kipindi cha sikukuu kama hivi huwa nina weka malengo ya jinsi gani ninaweza kujiendeleza au kubadilisha jinsi ninavyoishi maisha yangu. Haya malengo huwa natamani yaguse kila kinachohusiana na maisha yangu. Na haswa leo tunapokumbuka kufufuka kwa Bwana na mwokozi wa maisha yetu nimejiwekea malengo ya jinsi ninavyotaka kukua kiroho. Naomba Mungu niyatimize malengo yangu.
Pia unaweza kujiunganisha na marafiki zako nao ukasoma nao, lakini pia unapata mistari ya Biblia ya kila siku yenye picha ambazo unaweza ukawatumia marafiki zako. Pia unaweza kusoma Biblia kwa mwaka mzima kwani kuna masomo, mistari na alarm ya kukumbusha katika jambo hilo la kusoma Biblia kwa mwaka mzima. Zaidi ya haya yote mazuri kuna tafsiri mbalimbali za Biblia,unachagua ipi unayotaka kuisoma na ipi kwako ni rahisi.Kuna NIV,Swahili Bible, Amplified na nyingine nyingi. Kwasasa mimi natumia Good News Bible Translation.
Kwahiyo hii app inatuonyesha kwa ukaribu gharama na shida wanazopitia wakristo wenzetu kwenye mataifa mbalibali. Kila siku wanaweka nchi ya kuiombea, wanaielezea, lakini pia wanaweka ushuhuda wa kututia moyo kiimani kutokana na mambo ya kishujaa ambayo wakristo hao wamefanya hata katika mateso yao, lakini pia wanaweka interview (podcast) na watu hao au viongozi mbalimbali wa umisheni na wanaeleza mambo wanayokutana nayo.
Hiyo ndio zawadi yangu kwako ya Pasaka, Mungu akubariki sana na ukapate kufurahia kutumia hizi app na zikakusaidie kukua kiroho kama vile nilivyokusudia na ninavyoomba zinisaidie mimi.
6 Comments
Jacob Mushi
Nice thank you
Jacob Mushi
Nice thank you
Eunice Tossy
Welcome brother…
Thank you for visiting my blog
Pingback:
Pingback:
Pingback: